WANAHARAKATI WAANDAMANA KUPINGA MSWADA WA FEDHA 2024
Wanaharakati wamejiandaa kwa maandamano ya siku ya leo katika Wilaya ya Biashara ya Kati ya Nairobi kupinga mapendekezo ya Mswada wa fedha wa mwaka 2024.
Maandamano hayo yaliyopewa jina la Occupy Parliament yanatarajiwa kufanyike nje ya majengo ya bunge la kitaifa.
Mmoja wa waandalizi Boniface Mwangi amesema Wakenya kutoka kila sehemu ya nchi watakutana katika maeneo mbalimbali ya jiji kabla ya kuandamana hadi Bungeni.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































