MHUDUMU WA BODA BODA, ABIRIA WAFARIKI BOMET
Mhudumu mmoja wa boda boda na abiria wake wamefariki dunia kufuatia ajali kaunti ya bomet.
Ajali hiyo imefanyika katika eneo la chebole barabara kuu ya Bomet-Kapulonga, wakati lori lililokuwa likitokea upande wa pili lilimgonga dereva wa pikipiki na abiria wake.
Akithibitisha kisa hicho kamanda wa polisi kaunti ndogo ya bomet ya kati Ali Bashir amesema wawili hao wamefariki dunia papo hapo.
Miili yao ilipelekwa katika hifadhi ya mahiti ya hosipitali ya rufaa ya Longisa.
Imetayarishwa na: Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































