MUDAVADI KUZINDUA UTEUZI WA RAILA KWA UENYEKITI WA AUC NCHINI ETHIOPIA
Waziri Mkuu Musalia Mudavadi ataongoza rasmi ujumbe wa Kenya kwenda Addis Ababa, Ethiopia kwa uzinduzi wa uteuzi wa aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kwa nafasi ya Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).
Kulingana na taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Waziri Mudavadi amesafiri kwenda Ethiopia usiku wa kuamkia leo kuongoza hafla ya kuwahamasisha viongozi wa balozi zote ndani ya AU ili kumuunga mkono mgombea wa Kenya.
Kampeni hiyo inafuatia uidhinishaji wa Rais William Ruto wa Odinga kama kiongozi anayefaa kuongoza AUC mnamo Agosti 27, 2024.”
Uchaguzi wa AUC utafanyika Februari 2025 wakati wa Mkutano wa Umoja wa Afrika nchini Ethiopia ambapo wakuu wa nchi watapiga kura kumchagua mgombea anayefaa kumrithi mwenyekiti wa sasa Moussa Faki.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































