SERIKALI ITAGHARAMIKA SHILINGI BILIONI 30 KUKARABATI BARABARA

Waziri wa uchukuzi Kipchumba Murkomen amesema serikali itagharamika kati ya shilingi bilioni 25 hadi bilioni 30 katika kukarabati miundomsingi ya uchukuzi iliyoharibiwa na mafuriko.
Akizungumza katika kaunti ya Lamu alikozuru kutathmini barabara zilizoharibika katika kaunti hiyo, Waziri Murkomen amekiri kutatizika kwa hali ya usafiri kote nchini kutokana na mafuriko.
Amesema kwamba nyingi ya miundomisingi iliyoathirika zaidi ni daraja.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































