ALIYEKUWA WAZIRI MKUU RAILA AFARIKI
Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 80.
Kiongozi huyo wa chama cha ODM amefariki mapema leo katika hospitali moja jijini Kochi nchini India, alikokuwa akitibiwa kwa siku 5 zilizopita.
Odinga ambaye amekuwa kiongozi wa upinzani na mbunge wa Lang’ata hadi mwaka 2013, atakumbukwa kwa harakati zake za kuleta mageuzi nchini ikiwemo katiba ya mwaka 2010.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































