MADAKTARI KUTRH WAGOMA, WATATIZA MATIBABU
Shughuli za matibabu katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya chuo kikuu cha Kenyatta zimesambaratika kufuatia mgomo wa madaktari hospitalini humo ambao umeanza hii leo.
Madaktari hao wanalalamikia kusitishwa kwa bima ya afya na kile wanachokitaja kuwa usimamizi mbaya wa hospitali hiyo, na kutishia kusitisha huduma zote iwapo malalamishi yao hayataangaziwa.
Kulingana nao, kaimu afisa mkuu Isaac Kamau ndicho chanzo cha masaibu yao, na hivyo anafaa kutimuliwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































