UPINZANI KUKAMILISHA ZIARA YA MAGHARIBI
Viongozi wa upinzani wameratibiwa kukamilisha ziara yao ya siku 2 katika eneo la Magharibi mwa nchi hii leo, ambako wamekuwa wakiwataka wakazi wa eneo hilo kuwaunga mkono kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Miongoni mwa viongozi hao ni Rigathi Gachagua wa DCP, Kalonzo Musyoka wa Wiper, Eugene Wamalwa wa DAP-K na aliyekuwa waziri wa usalama Fred Matiang’i, wanaosisitiza kuhakikisha kuwa Rais William Ruto hapati muhula wa pili.
Wamewataka wakazi kuungana ili kuleta mabadiliko uongozini.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































