WAZEE EMBU WADAI HONGO KATIKA KUMTIMUA GACHAGUA

Wabunge na maseneta wameendelea kushutumiwa kwa madai ya kupokezwa hongo kabla ya kumbandua kutoka mamlakani naibu rais Rigathi Gachagua, licha ya masuala yenye uzito yanayolikabili taifa.
Wa hivi punde kuibua madai hayo ni wazee wa jamii ya Embu, ambao wamewashutumu wabunge kwa madai ya ubinafsi.
Wakiongozwa na Fundi Jacob, wazee hao wamewataka wabunge kutoa kipaumbele kwa hamasisho kuhusu bima mpya ya afya ya jamii SHIF.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa