MATIANG’I AHIMIZA MAZUNGUMZO
Waziri wa zamani Dr. Fred Matiang’i, amehimiza mazungumzo ya kitaifa kufanywa katika juhudi za kudhibiti machungu ya vijana na kurejesha mshikamano wa taifa.
Kulingana naye, serikali imefeli kuwasikiliza vijana, hatua anayosema huenda ikaligawanya taifa.
Naye kiongozi wa chama cha DCP Rigathi Gachagua, ameishutumu serikali kutokana na jinsi ilivyowashughulikia waandamanaji Jumatano iliyopita.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































