SIKU KUBWA UGANDA
Mamilioni ya raia nchini Uganda wameratibiwa kushiriki uchaguzi mkuu hii leo huku viongozi wa upinzani na wanaharakati wakiibua madai ya uwepo wa njama ya udanganyifu kwenye uchaguzi huo hasa kutokana na na kuzimwa kwa mitandao ya mawasiliano.
Rais Yoweri Museveni analenga kuendeleza utawala wake wa zaidi ya miaka 40 anapomenyana na mpinzani wake Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine kwenye uchaguzi huo.
Kulingana na upinzani, njama ya wizi inapangwa kutumiwa kwenye vifaa vya kielektroniki vya kupiga kura.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































