#Local News

TAHARUKI YAJITOKEZA CBD NAIROBI

Taharuki imeshuhudiwa katika eneo la biashara katikati ya jiji la Nairobi, CBD, baada ya polisi kuingilia kati maandamano ya wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma.

Maafisa wa polisi wameonekana wakiondoa vizuizi barabarani na kung’oa nambari za magari ya matatu yaliyokuwa yameegeshwa katika barabara kuu, huku wakijaribu kurejesha hali ya kawaida ya usafiri jijini.

Maandamano hayo ni sehemu ya malalamishi ya wahudumu wa matatu wanaodai serikali imeshindwa kuwalinda dhidi ya mashambulizi ya umati, hasa visa ambapo waendesha boda boda huharibu au kuchoma matatu kufuatia ajali za barabarani.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

TAHARUKI YAJITOKEZA CBD NAIROBI

SHARKS WATOKA HATARINI FKF

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *