EACC YAMNASA CHIFU KAKAMEGA
Tume ya maandili na kukabili ufisadi EACC imemkamata chifu wa kata ya Marama Central kaunti ya Kakamega Patrick Oyalo kwa madai ya kuitisha hongo ya shilingi elfu 10 kutoka kwa familia moja ili ipate hatimiliki ya shamba baada ya kifo cha baba wa familia hiyo.
Hatua hiyo imejiri chini ya siku moja baada ya EACC kuwasilisha ripoti kuhusu kiwango cha ufisadi nchini, ikiorodhesha afisi za machifu kama baadhi ya maeneo ambako uovu huo umeenea.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































