TUMEWAAJIRI WAKENYA ELFU 400, SERIKALI
Serikali ya Kenya Kwanza imewaajiri wakenya takribani elfu 400 wakiwemo walimu elfu 76,000, huku mikakati zaidi ikiendelea kuwekwa ili kuongeza nafasi za ajira.
Haya ni kulingana na naibu Rais Kithure Kindiki, akiongeza mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu umetoa nafasi elfu 200 huku wakenya zaidi wakiajiriwa kupitia mitandaoni.
Ameyasema haya alipopokezwa ripoti za taasisi mbali mbali za serikali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































