ZAIDI YA 1,000 WAANGAMIA SUDAN
Idadi ya watu walioangamia kwenye mmonyoko wa ardhi katika mlima wa Marra magharibi mwa Sudan imefikia zaidi ya 1,000 na kumuacha mwathiriwea mmoja pekee.
Haya ni kwa mujibu wa vuguvugu la Sudan Liberation Army, ambalo limetoa wito kwa umoja wa mataifa na jamii ya kimataifa kutoa msaada wa dharura ikiwemo uokoaji na utafutaji wa miili.
Mkasa huo ulitokea mwishoni mwa mwezi jana baada ya mvua kubwa katika eneo hilo liliko kwenye jimbo la Darfur.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































