DENI KUATHIRI MASOMO YA GREDI YA 10
Huenda masomo ya wanafunzi wa gredi ya 10 mwaka ujao yakatatizika kutokana na ukosefu wa vitabu, ambavyo wachapishaji wanasema hawajachapisha hadi sasa kutokana na deni la shilingi bilioni 11.4 wanalodai serikali.
Kupitia kwa muungano wao, wachapishaji wamesema deni hili litaathiri uchapishaji na usambazaji wa vitabu hivyo, wakiitaka serikali kulipa deni hilo.
Nakala milioni 7 za vitabu hivyo zimeratibiwa kuchapishwa, zoezi wanalosema huchukua miezi 2 huku usambazaji ukichukua mwezi mmoja.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































