SERIKALI YATOA BILIONI 18 ZA KUJENGA MADARASA YA GREDI 9

Juhudi za ujenzi wa madarasa 16,000 kwa wanafunzi wa gredi ya 9 ambao wanaanza masomo yao mwaka ujao zimepigwa jeki baada ya serikali kutoa shilingi bilioni 18.8 za kuwezesha ujenzi huo.
Akithibitisha kutolewa kwa fedha hizo, Waziri wa Elimu Julius Ogamba ametoa hakikisho kwamba serikali imejitolea kuhakikisha kuwa madarasa hayo yanakamilika kwa wakati ili kufanikisha masomo hayo.
Ameongeza kuwa wanashirikiana na hazina ya NG-CDF, hazina hiyo ikipewa jukumu la kujenga madarasa 5,000 huku yaliyosalia yakijengwa na wizara ya elimu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa