EACC YAREJESHA ARDHI YA UMMA
Tume ya kukabili ufisadi EACC imefaulu kurejesha vipande 12 vya ardhi ya umma iliyokuwa imenyakuliwa katika kaunti za Kakamega, Bungoma na Busia.
Akizungumza huko Mumias meneja wa EACC tawi la magharibi Eric Ngumbi anasema ardhi hizo zilichukuliwa na watu binafsi wakishirikiana na wafanyikazi wa serikali.
Anasema kwa sasa wanafuatilia vipande vingine 56 vinavyoaminika kutwaliwa na vinavyomilikiwa na idara tofauti za serikali ikiwemo ile ya makaazi mahakama na mamlaka ya viwanja vya ndege.
Imetayrishwa na Antony Nyonesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































