#Local News

RAILA AJIPIGIA DEBE KUWA MWENYEKITI WA AU HUKO ZANZIBAR

Kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga ameendeleza kampeni za kuwania wadhifa wa mwenyekiti wa umoja wa africa AU huko Zanzibar ambapo alihudhuria kongamano la mawaziri wa jumuiya ya afrika mashariki.

Akizungumza katika kongamano hilo Odinga amesema kuwa afrika ina nafasi nyingi sana za kujiimarisha kiuchumi na vile vile kujiendeleza kama bara huku akishinikiza kupanuliwa kwa mbinu za usafiri kupitia anga ,barabara na bahari ili kufungua mipaka ambayo kwa sasa inawazuia waafrika kutangamana inavyostahili.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *