MWANGA WA USALAMA KERIO
Walimu katika bonde la Kerio wamepongeza operesheni ya usalama
inayoendelea katika maeneo hayo wakisema kuwa hatua hiyo
imerejesha imani miongoni mwa wanafunzi na kufufua mahudhurio
shuleni.
Katibu wa muungano wa walimu KNUT, tawi la Elgeyo Marakwet John
Chebari amesema kuwa zaidi ya shule 35 ambazo zilikuwa zimefungwa au
kuathirika kwa visa vya uhalifu zinatarajiwa kurejelea shughuli za kawaida.
Hata hivyo, Chebari ameitaka serikali kudumisha hatua za sasa za
usalama ili wanafunzi wafurahie masomo kama wenzao na shughuli za
kawaida pia zirejelewe katika maeneo hayo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 









































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































