FORD KENYA YAKANA KUVUNJWA
Chama cha Ford Kenya kimepinga madai ya kuvunjiliwa mbali na kujiunga na kile tawala cha UDA, na kusisitiza kwamba mizizi yake katika siasa za humu nchini ni imara.
Kupitia kwa katibu wake mkuu ambaye pia ni mbunge wa Tongaren John Chikati, Ford Kenya imesema kwamba haina mpango wa kujiunga na UDA na badala yake kusisitiza kwamba kingali imara.
Chikati alikuwa ameandamana na viongozi wengine akiwemo naibu kinara wa chama hicho ambaye pia ni gavana wa Bungoma Ken Lusaka.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































