#Local News

GAVANA WA SIAYA JAMES ORENGO AMTAKA RAIS RUTO KUJIUZULU

Gavana wa Siaya James Orengo sasa anamtaka Rais William Ruto kujiuzulu akishikilia kuwa kuna hasira nyingi za umma dhidi ya serikali ya Kenya Kwanza.

Kwa mujibu wa Orengo iwapo Rais Ruto angesikiliza hisia za watu nchini, angeweza kujiuzulu kwa sababu Wakenya wamechoshwa na utawala uliopo.

Kufuatia kutupiliwa mbali kwa Mswada wa Fedha wa 2024 ambao haukupendwa na watu Orengo amesema ni lazima Wakenya wajiandae kwa nyakati zijazo.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *