OGAMBA AHAKIKISHA SULUHU LIPO
Waziri wa Elimu Julius Ogamba ameonyesha matumaini kwamba mazungumzo baina ya wizara hiyo na muungano wa KUPPET yatazaa matunda, na kuongeza kuwa serikali imetekeleza kikamilifu awamu ya pili ya mkataba wa maelewano na walimu.
Katika taarifa kwa wanahabari, Ogamba amesema kuwa masuala mengine yanaangaziwa na tume ya kuwaajiri walimu TSC
Aidha, amesema licha ya ukosefu wa baadhi ya walimu shuleni, wanafunzi wanaendelea kuripoti katika shule zao kote nchini.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































