SEKTA YA MIFUGO KUNUFAIKA KUPITIA MPANGO WA DRIVE

Sekta ya mifugo nchini imepata afueni baada ya Mpango wa DRIVE kutenga shilingi milioni 519 ili kupunguza hatari za ufugaji na kuongeza ushirikishaji wa jamii katika kuongeza thamani ya bidhaa za mifugo. Mpango huu unaoongozwa na Shirika la Maendeleo la Kenya (KDC) kwa usaidizi wa Benki ya Dunia, umezinduliwa jijini Nairobi katika mkutano wa wadau […]

POLISI WAMKAMATA DEREVA ALIYEMSAFIRISHA MUUAJI WA MBUNGE WERE

Polisi wanaendeleza uchunguzi baada ya kumkamata Amos Barasa Kasili, dereva wa bodaboda anayedaiwa kumsafirisha mshukiwa aliyempiga risasi Mbunge wa Kasipul Charles Were mnamo Aprili 30. Kasili amekamatwa Kibera baada ya uchunguzi wa kielelezo kuthibitisha uwepo wake eneo la tukio. Pikipiki yake inalingana na ile iliyorekodiwa kwa CCTV ikifuatilia gari la mbunge huku DCI ikihusisha mauaji […]

WAKAZI WA ASHABITO KUNUFAIKA NA HUDUMA MPYA ZA UMMA

Wakazi wa kaunti ndogo ya Ashabito, kaunti ya Mandera, sasa wataanza rasmi kupokea huduma za umma karibu nao kufuatia uzinduzi wa rasmi wa huduma hizo na serikali, Hafla iliyoongozwa na Waziri wa Utumishi wa Umma, Geoffrey Ruku, ambaye ameahidi kuanzishwa kwa kituo cha Huduma Center katika mji wa Rhamu, kitakachohudumia wakazi wa Ashabito na Mandera […]

MURKOMEN: SERIKALI KUDHIBITI WIZI WA MIFUGO MARSABIT NA ISIOLO

Baadhi ya maafisa waandamizi wa usalama wakiongozwa na Waziri wa Usalama Kipchumba Murkomen wanatarajiwa kufanya mikutano hii leo katika kaunti za Marsabit na Isiolo ili kuweka mikakati ya kudhibiti hali ya usalama kufuatia ongezeko la visa vya wizi wa mifugo. Waziri Murkomen amesema serikali imedhamiria kukabiliana vilivyo na wahalifu na kuhakikisha amani inarejea katika maeneo […]

KARUA AILAUMU TUME YA MAHAKAMA KWA KASORO KUU MAHAKAMANI

Tume ya Huduma za Mahakama inapaswa kubeba lawama kutokana na kasoro zinazoshuhudiwa katika Mahakama ya Upeo. Hayo ni kwa mujibu wa kiongozi wa chama cha Peoples Liberation Party (PLP), Martha Karua, ambaye anadai kuwa baadhi ya maafisa wanaohudumu katika tume hiyo hawana sifa stahiki, huku wengine wakidaiwa kuteuliwa kwa njia za kifisadi. Imetayarishwa na Janice […]

GOODISON PARK KUWAHUDUMIA WACHEZAJI WA EVERTON WANAWAKE

Uwanja wa Goodison Park utakuwa makao mapya ya timu ya wanawake ya Everton kuanzia msimu ujao, baada ya timu ya wanaume kuhamia uwanja mpya wa Bramley-Moore Dock. Badala ya kubomolewa, uwanja huo wa kihistoria utahifadhiwa kwa ajili ya Ligi Kuu ya Wanawake. Hii itaufanya kuwa uwanja mkubwa zaidi wa soka unaotumiwa na timu ya wanawake […]

KOCHA WA TUSKER AFUTILIA MBALI SABABU YA KUKOSEKANA KWA OGAM

Kocha wa Tusker FC Charles Okere amesema kuwa kutokuwepo kwa mfungaji wao nyota Ryan Ogam si sababu ya ukame wa mabao katika timu hiyo. Ogam, ambaye amefunga mabao 15 msimu huu, amekuwa nje kwa miezi mitatu kutokana na jeraha la goti. Tangu aumie, Tusker wamefunga mabao sita pekee katika mechi saba. Hata hivyo, Ogam amerudi […]

MCHEZAJI BARNABAS OWUOR KUAGANA NA STRATHMORE LEOS

Barnabas Owuor, mchezaji wa Strathmore Leos, ametangaza kuwa msimu huu utakuwa wa mwisho kwake kuichezea timu hiyo baada ya kuhudumu kwa zaidi ya miaka kumi. Tangazo hilo linahitimisha kipindi cha dhahabu kwa mmoja wa wachezaji wenye ushawishi mkubwa katika timu hiyo ya chuo kikuu. Safari yake ya mchezo wa raga ilianza katika Shule ya Upili […]

KENYA YALENGA KUONGEZA MARA NNE MAUZO YA CHAI CHINA KUFIKIA 2030

Serikali ya Kenya imelenga kuongeza mara nne na zaidi mauzo ya chai nchini China ndani ya miaka sita ijayo. Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo na Mifugo, Mutahi Kagwe, ambaye amesema kuwa lengo ni kupandisha mauzo kutoka kilo milioni 12.42 mwaka huu wa 2024 hadi kufikia kilo milioni 50 ifikapo mwaka 2030. Kagwe ametoa taarifa […]

MFUMO MPYA WA KILIMO WAINUA WAKULIMA WADOGO AFRIKA MASHARIKI

Kenya imetajwa kuwa kielelezo barani Afrika katika kuwezesha upatikanaji wa mikopo kwa wakulima wa mashamba madogo madogo, kufuatia mafanikio ya majaribio ya mfumo wa kifedha uliotekelezwa kwa kushirikiana kati ya Hello Tractor, na Heifer International. Kupitia mfumo wa lipa kadri unavyotumia kwa matrekta, wakulima na wajasiriamali wamepata fursa ya kujiendeleza kwa kutumia mashine bila kuhitaji […]