MHASIBU WA MAGEREZA GEREZANI

Aliyekuwa mhasibu wa serikali katika idara ya huduma za magereza Humphrey Abok ameshtakiwa kwa ulaghai wa mali ya umma yenye thamani ya shilingi milioni 302.
Abok na washukiwa wenza wanatuhumiwa kuilaghai serikali kwa kupokea malipo ya bidhaa ambazo kamwe hazikutolewa.
Abok amekanusha mashtaka dhidi yake na kuachiliwa kwa dhamana ya shilingi milioni saba au dhamana mbadala ya pesa taslimu shilingi milioni nne.
Kesi hiyo itatajwa tena tarehe tatu mwezi septemba mwaka huu.
Imetayarishwa na Nelson Andati