“HATUWATAMBUI!” WAANDAMANJI BUNGOMA

Vijana kutoka maeneo bunge ya webuye magharibi na webuye mashariki kaunti ya Bungoma wameandamana mjini Webuye huku wakiwakosoa wabunge wao ambao ni Dan Wanyama na Martin Wanyonyi kwa kupiga kura ya ndio kuhusu mswada wenye utata juma lililopita.
Wakati wa maandamano hayo, kijana mmoja aliyejitokeza kupinga maandamano hayo amejeruhiwa vibaya na waandamanaji.
Aidha, vijana hao wamelalamikia hali ngumu ya Maisha, wakiapa kuendelea na maandamano hayo hadi kilio chao kitakaposikilizwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa.