RUTO: AFRIKA HAITAKUBALI KUBAGULIWA UN
Rais William Ruto amewahimiza viongozi wa Afrika kuungana katika juhudi zao za kushinikiza mageuzi katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.
Rais ambaye yuko jijini New York kuhudhiria kikao cha 80 cha baraza kuu la umoja wa mataifa maarufu kama UNGA, amesema haitakubalika kwa Afrika kuendelea kubaguliwa katika baraza hilo.
Amewataka viongozi hao kushinikiza kupitia ushirikiano wao wa taifa kwa taifa au hata kikanda ili kuleta mageuzi hayo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































