MBINU ZA SERIKALI DHIDI YA MAANDAMANO

Wawakilishi wa kike wanaoegemea mrengo wa Kenya Kwanza wameanza kuzuru maeneo mbali mbali wakiwarai vijana kusitisha maandamano na kukubali mazungumzo na Rais William Ruto.
Wakizungumza na Beatrice Adagala wa Vihiga, viongozi hao wamesema maandamano yanaathiri uchumi, wakiwarai wazazi kuwashawishi wanao ili wampe rais muda wa kutekeleza matakwa yao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa