#uncategorized

SHUMAH ANG’ARA LIGI KUU ZAMBIA

Mshambuliaji wa Kenya Moses Shumah anaendelea kung’ara katika msimu wa 2025/2026 akiwa na klabu ya Power Dynamos FC ya Zambia, akijidhihirisha kama mmoja wa washambuliaji tegemeo kuelekea mashindano ya AFCON 2027.

Mchezaji huyo wa zamani wa Kakamega Homeboyz anaongoza orodha ya wafungaji katika MTN Super League ya Zambia akiwa na mabao 12 tangu ajiunge na klabu hiyo Julai 2025.

Shumah alionyesha kiwango cha juu Machi 8 baada ya kufunga mabao matatu katika ushindi wa mabao 3–2 dhidi ya mahasimu wao Zesco United, matokeo yaliyomuweka kileleni katika kinyang’anyiro cha kiatu cha dhahabu.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

SHUMAH ANG’ARA LIGI KUU ZAMBIA

KATYWA AMUAMINI CANTONA KABRAS

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *