OGAMBA ATOA AGIZO KWA WAKUU WA VYUO VIKUU

Waziri wa elimu Julius Ogamba amesema kila mwanafunzi aliyefuzu kujiunga na chuo kikuu ataruhusiwa kuanza masomo yake licha ya kukosa kulipa karo inayohitajika kulipwa na mzazi, na kwamba wanafunzi watapewa fursa katika vyuo walivyochagua wenyewe.
Kulingana na Waziri huyo, wizara ya elimu imewaagiza wakuu wa vyuo vikuu vya umma kuwasajali wanafunzi wote bila ubaguzi wowote, mbali na kuhakikisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanapata makazi.
Aidha, Ogamba amesema wizara yake inashirikiana na wizara ya fedha kuona kwamba ufadhili wa masomo unatumwa kwa wakati mwafaka.
Imetayarishwa na Janice Marete