“SITAKI KUITWA ZAKAYO PEKEE YANGU” RUTO
Rais William Ruto amesema kwamba lengo lake la kubuni serikali pana kwa ushirikiano na mrengo wa upinzani ni kuliunganisha taifa ili kuafikia mageuzi ya kiuchumi.
Akizungumza katika eneo la Rukuriri kaunti ya Embu, Rais amesema hatua hiyo itadhibiti kauli za uchochezi na kutoa fursa kwa taifa kuangazia ajenda yake ya maendeleo.
Aidha, amesema kupitia serikali pana, taifa linaweza kukusanya ushuru kwa Pamoja bila yeye kubebeshwa lawama binafsi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































