IDADI YA VIFO KUTOKANA NA MAFURIKO NI 299, KITHURE ASEMA

Waziri wa usalama wa kitaifa Kithure Kindiki amesema kuwa jumla ya watu 299 wamefariki kutokana na mafuriko hapa nchini, 75 wasijulikane waliko huku wengine 188 wakiuguza majeraha.
Kulingana na Kindiki, mafuriko hayo yamewaathiri familia 55,631, huku jumla ya watu 278,155 wameathirika.
Aidha, kambi 187 zimewekwa katika kaunti 25 kote nchini kuwapa hifadhi waathiriwa, kaunti ya Busia ikiwa miongoni mwa kaunti zilizoathirika pakubwa ndani ya saa 24 zilizopita.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































