POLISI WALIOKABILI WAANDAMANAJI HAWAKUPEWA CHAKULA,YASEMA IPOA
Polisi waliotumwa kukabili waandamanaji wakati wa maandamano ya Juni 25 na Julai 7 hawakupewa chakula na maji ya kutosha.
Mamlaka ya kuangazia utendakazi wa polisi Ipoa inasema maafisa hao waliotumwa kutoa ulinzi kwa majengo na taasisi za serikali maslahi yao hayakuangaziwa ipasavyo.
Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja ametakiwa kuhakikisha bajeti ya kutosha imewekwa kushughulikia polisi wanaotumwa nje wakati wa maandamano.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































