RAIS AONYA WABUNGE NA MASENETA WAFISADI
Rais William Ruto ameonya kuwa wabunge na maseneta wanaojihusisha na ufisadi kwa kuitisha pesa kutoka kwa maafisa wa serikali wanaofika mbele yao watachukuliwa hatua.
Akiongea wakati a mkao wa pamoja wa wabunge wa chama cha UDA na ODM rais anasema amepokea habari kuhusu sakata za ufisadi zinazoendelea katika bunge la taifa na lile la seneti.
Rais ametaja kisa cha hivi punde ambapo maseneta walipokea kiasi cha shilingi milioni 150 ili kumpendelea afisa aliyefika mbele yao.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































