HISIA ZA MSAMAHA WA RUTO
Rais William Ruto alistahili kuzuru hospitali ya Kenyatta wanakotibiwa waathiriwa wa maandamano ya kizazi cha Gen Z mwaka jana na kuwalipia bili za hospitali kama njia mwafaka ya kuwaomba msahama.
Ndiyo kauli ya seneta wa Makueni Dan maanzo, akirejelea msahama alioomba rais hapo jana kupitia runinga.
Hata hivyo, aliyekuwa kiongozi wa wengi katika bunge la seneti Samuel Poghisio, amemtea rais akitaja hatua hiyo kuwa unyenyekevu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































