#Local News

MAKALI AOMBA SUBIRA KWA WAFANYAKAZI WA SUKARI

Mbunge wa Kanduyi John Makali amewaomba wafanyakazi wa viwanda vya sukari katika mkoa wa Magharibi kuwa na subira huku serikali ikiendelea kushughulikia ulipaji wa malimbikizi ya mishahara yao.

Akizungumza katika kaunti ya Bungoma, Makali ametoa hakikisho kuwa serikali iko mbioni kuhakikisha wafanyakazi pamoja na wakulima wa miwa wanalipwa fedha wanazodai kwa wakati unaofaa.

Hata hivyo, amewasuta baadhi ya watu anaodai wanatumia suala hilo kuchochea vurugu na maandamano, akisema hatua kama hizo haziwezi kusaidia kutatua changamoto zinazokumba sekta ya sukari.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

MAKALI AOMBA SUBIRA KWA WAFANYAKAZI WA SUKARI

WAZOA TAKA DANDORA WASHINDA KESI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *