#Local News

AJALI YA BODA BODA YAUA MWANAMKE BUSIA

Mwanamke mwenye umri wa makamo ameaga dunia kufuatia ajali ya barabarani iliyohusisha boda boda katika eneo la Mlango Kumi, kwenye barabara kuu ya Busia kuelekea Kisumu.

Ajali hiyo ilitokea mapema hii leo, huku chanzo chake kikisalia kutambuliwa na maafisa wa polisi waliowasili eneo la tukio kufanya uchunguzi.

Abiria wengine wawili waliojeruhiwa katika ajali hiyo walikimbizwa katika hospitali ya kibinafsi Bulanda, Kaunti ya Busia, kwa matibabu ya dharura.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *