#Local News

MAHANGAIKO ZAIDI VYUONI KUFUATIA MGOMO

Shughuli za masomo zimeendelea kutatizika katika vyuo vikuu vya umma nchini kwa wiki ya 4 sasa kufuatia mgomo wa wahadhiri ambao hii leo wameandamana jijini Nairobi na kuelekeza malalamishi yao katika majengo ya bunge, wizara ya fedha na ile ya elimu.

Wakiongozwa na katibu mkuu wa muungano wa UASU Daktari Constantine Wasonga na mwenyekiti Grace Nyongesa, wahadhiri hao wameshikilia kuwa hawatarejea kazini hadi maslahi yao yatakatapotimizwa.

Miongoni mwa malalamishi yao ni nyongeza ya mishahara, bima ya afya na kuajiriwa kwa wafanyakazi Zaidi.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

MAHANGAIKO ZAIDI VYUONI KUFUATIA MGOMO

WAPE MTIHANI KAMA WAKO SAWA, OGAMBA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *