MGOMO WA MADAKTARI WANUKIA KERICHO
Huenda shughuli za matibabu katika kaunti ya Kericho zikatatizika ndani ya wiki mbili zijazo iwapo serikali ya kaunti hiyo haitaingilia kati na kusitisha mgomo wa madaktari ambao wametoa notisi ya siku 14.
Kupitia taarifa, viongozi wa muungano wa KMPDU wameilaumu serikali ya kaunti hiyo kwa madai ya kukosa kutekeleza mpango wa huduma uliokubaliwa, mfumo wa kurejea kazini uliotiwa Saini mwaka 2023 miongoni mwa malalamishi mengine.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































