WAKAZI KIRINYAGA KUKOSA HUDUMA ZA BUNGE LAO

Wakazi katika kaunti ya Kirinyaga watalazimika kukosa huduma za bunge la kaunti hiyo baada ya vikao vya bunge hilo kuahirishwa kwa muda kufuatia mzozo wa uongozi ulioshuhudiwa hapo jana.
Haya yanajiri baada ya makundi mawili bungeni humo kukosa kuafikiana kuhusu pendekezo la kumtimua kiongozi wa walio wengi Muriithi Kibinga ili kujaza nafasi yake na Geoffrey Murimi.
Hata hivyo, katibu mkuu wa chama cha UDA Hassan Omar amesitisha mageuzi katika chama hicho kwenye kaunti ya Kirinyaga hadi mkutano na wawakilishi wadi tarehe 28 mwezi huu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa