#Football #Sports

BARCELONA YAMSAJILI CHIPUKIZI AJAY TAVARES

Klabu ya FC Barcelona imemsajili mchezaji chipukizi Ajay Tavares kutoka akademi ya Norwich City.

Tavares, mwenye umri wa miaka 16, anaripotiwa kuvutia vilabu kadhaa barani Ulaya. Norwich itapokea fidia ya malezi, ingawa haijathibitisha kiasi cha fedha kinachohusika katika makubaliano hayo.

Mchezaji huyo alijiunga na Norwich akiwa chini ya umri wa miaka 12. Msimu uliopita alitokea benchi katika mechi ya kirafiki ya kujiandaa na msimu mpya dhidi ya klabu ya Uholanzi, FC Volendam, akiwa na umri wa miaka 15.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

BARCELONA YAMSAJILI CHIPUKIZI AJAY TAVARES

KATASI ANG’ARA LIGI KUU YA KPL

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *