UHABA WA MATABIBU WAATHIRI HUDUMA ZA AFYA

Uhaba wa matabibu nchini  umeathiri huduma za afya  kwa wakenya serikali ikitakiwa kuajiri wahudumu hao Zaidi. Wakiongea kwenye kongamano linaloendelea huko Mombasa wanasema  idadi ya wagonjwa wanaohudumiwa na tabibu mmoja iko juu zaidi ikilinganishwa na  kiwango kilichowekwa na shirika la afya duniani WHO. Wanasema kutokana na uhaba huo wagonjwa mara nyingi hutumwa katika vituo  vingine […]

KAMATI YA AFYA YAFIKA ELDORET KUCHUNGUZA BIASHARA YA FIGO

Kamati ya bunge kuhusu afya imezuru mji wa Eldoret kaunti ya Uasin Gishu kufanya uchunguzi katika madai ya kuendeshwa kwa biashara ya kuuza figo vinavyohusisha vijana wengi. Kamati hiyo imezuru Eldoret baada ya mbunge wa Nandi Hills Benard Kitur kuwasilisha hoja bungeni akisema vijana wengi wameathirika baada ya kuuza figo zao. Tayari watu wanaodaiwa kuuza […]

RAIS RUTO AAHIDI AFCON YA KUKATA NA SHOKA

Rais William Ruto Alhamisi aliahidi kwamba Kenya itaandaa michuano ya kukumbukwa ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, na hivyo kupata imani kutokana na nchi hiyo kuandaa vyema michuano ya Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024 pamoja na Uganda na Tanzania. Akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha mchana Ikulu iliyoandaliwa kwa heshima ya Harambee […]

DROO YA LIGI YA MABINGWA

Liverpool na Manchester City zote zitamenyana na Real Madrid katika Ligi ya Mabingwa msimu huu huku mabingwa watetezi Paris Saint-Germain wakipewa orodha ngumu ya wapinzani kwenye droo iliyofanywa jana ikiwa ni pamoja na Barcelona na Bayern Munich. Real ya Xabi Alonso itacheza na City nyumbani na kumenyana na mabingwa wa Premier League Liverpool katika uwanja […]

OSAMA AHAMIA MURANGA’ SEAL

Timu ya Ligi Kuu ya FKF (FKF-PL) Murang’a Seal imepata huduma ya nyota anayechipukia mwenye umri wa miaka 22 Paul Osama kutoka Mombasa United. Osama, ambaye alionyesha kiwango kizuri msimu uliopita akiwa na kikosi cha National Super League (NSL), alichukua jukumu muhimu katika kusaidia klabu kuepuka kushuka daraja. Uchezaji wake bora, ikiwa ni pamoja na […]

WAKENYA WAFAGIA JUKWA LA USHINDI

Bingwa mtetezi wa Olimpiki wa mbio za mita 800 Emmanuel Wanyonyi  alitua dhahabu  na kumshinda mpinzani wake wa karibu Max Burgin wa Uingereza na kutwaa Kombe la Diamond League, huku Wakenya wakitoa matokeo bora ya usiku wa mbio za riadha katika fainali ya mzunguko mjini Zurich mnamo . Wanyonyi, ambaye anaelekea kwenye Mashindano ya Dunia […]

WANGAMATI AAGIZWA KUKAMATWA

Aliyekuwa gavana wa Bungoma Wycliffe Wangamati na mbunge wa Webuye West Dan Wanyama, wamepata pigo baada ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma DPP kuidhinisha kwamba wafunguliwe mashtaka ya ufisadi unaohusisha ufujaji wa shilingi milioni 70.2. Fedha hizo zinaripotiwa kufujwa kupitia utoaji wa kandarasi kwa kampuni zilizo na uhusiano wa karibu na wawili hao ambao sasa […]

SIKU YA GAVANA MUTAI SENETI

Gavana wa Kericho Erick Mutai anatazamiwa kufahamu hii leo iwapo ataendelea kuwa gavana au la, kwenye uamuzi utakaotolewa kupitia kura ya maseneta ikiwa ni siku ya 3 na ya mwisho ya kusikiliza hoja ya kubanduliwa kwake. Wawakilishi wadi wa kaunti hiyo wameendelea kuishawishi seneti kudumisha uamuzi wao wa kumbandua, wakidai kwamba amefuja fedha za umma. […]

IEBC KUANZA USAJILI WA WAPIGA KURA

Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imetangaza kurejelea zoezi la kuwasajili wapiga kura wapya kuanzia Jumatatu wiki ijayo kote nchini. Kupitia taarifa, IEBC imesema wanaolengwa ni wakenya walio na umri wa miaka 18 au Zaidi na ambao hawakuwa wamesajiliwa kama wapiga kura, na wale wanaolenga kuhamishia maelezo yao katika vituo tofuati vya kupigia kura. […]

MAHAKAMA YAAGIZA KUSITISHA UJENZI WA KANISA KATIKA IKULU

Mahakama Kuu imetoa agizo la kusitisha kwa muda ujenzi wa majengo yoyote ya kudumu ya kidini, yakiwemo makanisa, katika Ikulu hapa Nairobi, na makazi mengine rasmi ya serikali kote nchini. Agizo hilo lilitolewa na Jaji Chacha Mwita kufuatia ombi kutoka kwa shirika la Transparency International Kenya, Tume ya kutetea Haki za Kibinadamu ya Kenya, na […]