MWANGI APANGA TAMASHA UHURU PARK KWA KUHESHIMU WAANDAMANAJI WALIOFARIKI

Mwanaharakati Boniface Mwangi anapanga tamasha la wazi bila malipo katika bustani ya Uhuru Park kuwaenzi waandamanaji wote walioaga dunia kwa kupigwa risasi walipokuwa wakitekeleza haki yao ya kidemokrasia ya kupinga mswada wa fedha.
Alipokuwa akishiriki mipango hiyo katika mtandao wa X, Mwangi amesema juhudi za kumfikia Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja zimegonga mwamba. Mwangi ameongeza kuwa simu zake kwa gavana na Shaffie Weru, ambaye ndiye msimamizi wa hafla hiyo katika kaunti hiyo, hazikupokelewa.
Imetayarishwa na Janice Marete