#Local News

NCIC; RIPOTI KESI ZA UCHOCHEZI

Tume ya Kitaifa ya Uwiano na Utangamano NCIC inachunguza visa 43 vya matamshi ya chuki yaliyoripotiwa kati ya Aprili na Juni mwaka huu huku ikilenga kuhimiza kuwepo kwa amani nchini.

Katika taarifa yake tume hiyo imesema kesi hizo ziko katika hatua mbalimbali za uchunguzi na kwamba ni sehemu ya ripoti 67 ambazo zimeripotiwa.

NCIC pia imehimiza umma kuripoti kesi zinazoweza kuchochea hisia za dharau, chuki, ghasia, ubaguzi na pia zile zinazoweza kuathiri amani nchini kupitia Huduma ya Ujumbe Mfupi (SMS) nambari 1547 bila malipo.

Imetayarishwa na Janice Marete

NCIC; RIPOTI KESI ZA UCHOCHEZI

RAIS RUTO ANATARAJIWA KUHUTUBIA TAIFA

NCIC; RIPOTI KESI ZA UCHOCHEZI

MAANDAMANO YALEMAZA BIASHARA BOMET

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *