LSK YATOFAUTIANA NA UAMUZI WA MAHAKAMA

Chama cha mawakili nchini LSK kimekosoa uamuzi wa Jaji Laurence Mugambi kwamba wanajeshi wa KDF wahusishwe katika kuwakabili waandamanaji.
Kwa mujibu wa rais wa LSK Faith Odhiambo utaratibu uliotumika kuwatuma wanajeshi hao ulikiuka katiba huku akisikitikia uamuzi wa mahakama.
Odhiambo amesema kuwa uamuzi wa jaji Mugambi huenda ukasababisha visa vya uvunjaji sheria.
Imetayarishwa na Nelson Andati