#uncategorized

MGOMO WAFUTILIWA MBALI MACHAKOS

Ni afueni kwa wakaazi wa Machakos baada ya maafisa wa kliniki kufutilia mbali mgomo wao uliopangwa kuanza usiku wa leo.

Hii ni baada ya maafisa wa muungano wa wahudumu hao kutia Saini mkataba wa maelewano na serikali ya kaunti ya Mchakos ukilenga kuangazia lalama walizoibua.

Kupitia mwenyekiti wao wa kitaifa Peterson Wachira wanasema miongoni mwa masuala hayo ni kupandishwa vyeo kwa maafisa ambao wamesalia katika kiwango kimoja kwa muda na kuongezwa kwa mshahara.

Imetayarishwa na Maureen Mukhobe

MGOMO WAFUTILIWA MBALI MACHAKOS

TAHADHARI YATOLEWA KUHUSU MPOX

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *