JAJI MUSTAAFU MUTUNGA NA KARUA WASHTAKI TANZANIA
Kuna haja ya wapatanishi kuingilia kati na kuondoa uhasama uliopo kati ya wanaharakati wa humu nchini na serikali ya tanzania.
Hii ni baada ya aliyekuwa jaji mkuu Willy Mutunga na mwanasiasa Martha Karua kuwasilisha kesi Katika mahakama ya haki ya afrika mashariki dhidi ya serikali hiyo kwa kosa la kuwazuilia kinyume na sheria na kuwazuia kuingia nchini humo.
Wanaharakati hao wakiwa pamoja na wengine Gloria Kimani Lynna Ngugi Hussein Khalid na Hanisa Adan wanataka msamaha kutoka kwa serikali ya Tanzania.
Imetayarishwa na Maureen Amakhobe
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































