MAHAKAMA YAHARAMISHA KARO YA ZIADA
Mahakama imewapa afueni wazazi kwa kurahamisha hatua za shule za umma kuwatoza ada za ziada bila idhini ya wizara ya elimu nchini.
Uamuzi huo wa mahakama unafuatia kesi iliyowasilishwa dhidi ya shule ya upili ya St. Georges iliyowataka wazazi kulipa ada za ziada, mahakama ikisema hatua hiyo na haramu.
Kwenye kesi hiyo, mahakama ilibaini kuwa shule hiyo iliwataka wazazi kugharamia masuala kadhaa ikiwemo ujenzi wa bweni na kufadhili mapungufu ya fedha kwenye bajeti ya shule.
Imetayrishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































