WAKULIMA MACHAKOS WAPATA ‘MBEGU ZA MATUMAINI’

Wakulima katika kaunti ya Machakos wamepata afueni baada ya serikali ya kaunti hiyo kuzindua mpango wa kuwapa mbegu za kupanda msimu huu wa mvua ya vuli.
Akizindua mpango huo katika eneo la Matuu, gavana Wavinya Ndeti amesema kuwa wanalenga wakazi walio na mapato ya chini kwa lengo la kuimarisha utoshelevu wa chakula.
Mbegu za mahindi, maharagwe na nyasi za mifugo zimeanza kusambazwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa