#Sports

VILABU MBIONI KUMALIZIA MIKATABA MIPYA

vilabu vya Arsenal, Chelsea, Manchester United na Liverpool vinajizatiti kupata sajili kubwa zaidi kwenye dirisha hili la uhamisho.

Arsenal sasa inasemekana wamefikia makubaliano na Benjamin Sesko, wakati bado wanaweza kumnunua Morgan Rogers huku Viktor Gyokeres akiripotiwa kuwa tayari kugoma kulazimisha kuondoka kwake. Walakini, wanaweza kuwakosa Rodrygo na Nico Williams.

Chelsea wanasemekana kuwa wamefanya mawasiliano juu ya kuipiku Newcastle kwa dili la Joao Pedro huko Brighton huku wakiendelea na mazungumzo juu ya Jamie Gittens na Mohammed Kudus, ingawa sasa wanakabiliwa na vita dhidi ya Malick Fofana na Liverpool, ambao watamkaribisha Florian Wirtz leo kwa sehemu ya kwanza ya vipimo vyake vya afya huku wakitarajia kufunga makubaliano ya Milos Kerkez.

Manchester United bado wanashinikiza kumnasa Bryan Mbeumo na wana nia ya kuwanunua Hugo Ekitike pamoja na Victor Osimhen.

Tottenham sasa wanaaminika kuwa wameondoa nia yao ya kumnunua Mbeumo, huku Leeds wakishuhudia ofa kubwa kwa Rodrigo Muniz kukataliwa na Fulham.Manchester United wanaonekana kuongezewa nguvu mpya zaidi ya Bryan Mbeumo.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon amekuwa msisitizo mkuu wa shughuli za uhamisho huko Old Trafford kufuatia mkataba wa mapema wa pauni milioni 62.5 kwa mshambuliaji wa Wolves Matheus Cunha.

United wanajaribu kufunga mkataba na Brentford baada ya kuona ofa ya ufunguzi yenye thamani ya jumla ya £55m ikiwa ni pamoja na nyongeza kukataliwa, ingawa ilionekana kukabiliwa na tishio jipya kutoka kwa Tottenham baada ya kumteua Thomas Frank kama meneja wao mpya.

Spurs wamekubali kushindwa na kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha kumnasa Mbeumo, ambaye inaonekana amewahi kuwa na macho tu kwa United.

Imetayrishwa na Nelson Andati

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *