MMOJA AUAWA KIMILILI, NYUMBA ZABOLEWA

Hali ya kawaida imeanza kurejea katika kijiji cha Kibingei eneo bunge la Kimilili kaunti ya Bungoma baada ya polisi kuwakamata washukiwa watatu kufuatia mauaji ya mwanamme mwenye umri wa miaka 34 eneo hilo kuhusiana na kinachoaminika kuwa mzozo wa kimapenzi.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi eneo la Kimilili Nzaka Mwitu, mwathiriwa kwa jina Ben Kisabuli alishambuliwa alipokuwa akiekea nyumbani na kujeruhiwa kabla ya kuaga dunia alipokuwa akitibiwa.
Hata hivyo, watu wasiojulikana walibomoa nyumba za washukiwa kwa lengo la kulipiza kisasi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa